Tanzania National Parks
@tzparks
Tanzania National Parks is a parastatal organization which has the mandate to manage all areas designated as National Parks . It manages 21 National Parks
ID:608826775
http://www.tanzaniaparks.go.tz 15-06-2012 06:09:12
2,7K Tweets
29,6K Followers
156 Following
Ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Arusha utakutana na Baboon wa kutosha kwa nyakati tofauti wakiwa na harakati zao tofauti tofauti. Hapa utaona mengi sana, fika hifadhini. Kikubwa hautakiwi kuwapa chakula, tazama video fupi wakiwa katika shughuli zao
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Anaitwa Pongo ni mnyama ambaye hupenda kuishi katika vichaka na huwa haonekani sana, naweza sema ni bahati kukutana naye nami nilibahatika kumuona, tembelea hifadhi ya Taifa ya Arusha utapata kumuona mnyama huyu kwa ukaribu
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Nilianza na Safari ya kutembea kwa Miguu na hapa nikapata historia ya mafuvu haya ya Nyati, ambapo picha ya pili ilikuwa ni Nyati dume kulingana na kuwa na pembe kubwa zilizopinda na picha ya tatu ni nyati jike, Tembelea Hifadhi ya Taifa ya Arusha
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Ni ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Arusha hifadhi hii ina misitu minene na miti iliyofungana mpaka kutengeneza giza fulani ambalo limekuwa sehemu ya kivutio kwa wewe ambaye utatembelea katika eneo hilo na unaweza kubahatisha kukutana na Chui akikatiza
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Nikiwa katika Hifadhi ya Taifa ya Arusha nilipata kufahamu umuhimu wa vibao na kama muongoza utalii vinamsaidia kufahamu maeneo sahihi ambayo mtalii anatakiwa tembelea maeneo mengine yanabaki kwa matumizi ya wahifadhi, ukitembelea utaeleweshwa zaidi
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Napenda kukutoa wasi wasi katika Hifadhi ya Taifa ya Arusha kuna Barabara nzuri na haya ni maeneo niliyopita nikiwa natalii, kongole kwa Tanzania National Parks kwa kuboresha miundombinu, unaweza kutembelea kipindi chote cha mwaka japo muda mzuri ni Juni mpaka Oktoba
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Kama nilivyoahidi takupitisha hatua kwa hatua uwapo katika Hifadhi ya Taifa ya Arusha kwa ajili ya kutalii, ukiwa hifadhini utaongozwa na alama za barabarani na cha kuzingatia ni speed 30KM/H pamoja na alama zote kama picha hizi nilizopiga hifadhini
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Niliposema Hifadhi ya Taifa ya Arusha ina miundombinu mizuri nilimaanisha, katika safari ya Mguu niliona madaraja mazuri ambayo ni salama pia ni maeneo bora ya kupigia picha , na hapa niwapongeze Tanzania National Parks kwa ubunifu ukifika utaelewa
Angellah Kairuki
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Ni kwa mara ya kwanza nikiwa katika Hifadhi ya Taifa ya Arusha nakutana na Nyati/Mbogo rafiki hawasumbui kwa namna yoyote na wanaona watu mara kwa mara hivyo wamekuwa rafiki wa binadamu, mimi niliwapiga picha nikiwa karibu nao kabisa tazama video.
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
'Twiga hawa wanajifunza kupigana' ni sauti ya Mhifadhi Dominic, alinieleza kuwa hii inawasaidia hata wanapokuwa wakubwa kuweza kukabiliana na adui aidha kupigana wao kwa wao. tazama namna wanavyopigana, nawe tembelea kuona mengi zaidi
Carol Ndosi
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Haya ni maporomoko ya maji Tululusia ni makubwa na yanayopatikana katika Hifadhi ya Taifa Arusha, baada ya matembezi hifadhini kwa miguu hii ni sehemu nzuri ya kupumzika,kwa maelezo ya zaidi tazama video hapa, karibu kutembelea Hifadhi hii
#Localtourtz
πΈ Fredy Njeje
Kupitia kampeni yangu inayokwenda kwa jina la #Localtourtz lengo kubwa ni kuwahamasisha watanzania wenzangu kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii Tanzania, inawezekana na kwa sasa hamasa yangu zaidi mtembelee hifadhi hii ya Taifa Arusha
π½ Fredy Njeje
Asanteni kwa wewe uliyefuatilia Safari yangu katika Hifadhi ya Taifa ya Arusha inayosimamiwa vema kabisa na Tanzania National Parks na sehemu ya kwanza imemalizika sasa kaa mkao wa kusubiri Game Drive huko utaona mambo mengi zaidi
Angellah Kairuki
Carol Ndosi
#Localtourtz
π½ Fredy Njeje
Karibu Tanzania, Karibu Hifadhi ya Taifa ya Arusha iliyo chini ya Tanzania National Parks nilifanikiwa kutembelea hifadhi hii, pamoja na yote nitakupitisha katika maeneo mbalimbali lengo ni kukupa hamasa na wewe kutembelea. Kuwa nami hapa mwanzo mwisho mambo mazuri yanakuja
#Localtourtz